Je ni vipi ambavyo kukomaa kwa hedhi kutaathiri mwili wangu

From Audiopedia - Accessible Learning for All
Jump to: navigation, search
QR for this page

https://www.audiopedia.org/Je_ni_vipi_ambavyo_kukomaa_kwa_hedhi_kutaathiri_mwili_wangu

Ishara moja ya kuzeeka kwa akina mama ni kuisha kwa siku za hedhi. Siku za hedhi zinaweza kuisha ghafla, au zinaweza kuchukua kati ya mwaka 1 hadi miaka 2. Kwa wanawake wengi, mabadiliko haya hufanyika kati ya umri wa miaka 45 na 55.

Ishara:

  • Siku zako za hedhi hubadilika. Wakati mwingine huisha ghafla, au utapata hedhi kwa muda. Au, hedhi itasimama kwa miezi kadhaa na kurudi tena.
  • Wakati mwingine, utahisi joto au kutokwa na jasho (kuwa na vipindi vya joto). Hii inaweza kukuamsha usiku.
  • Uke wako unakuwa mdogo na huitakuwa na unyevunyevu.
  • Hisia zako zitabadilika kila mara.

Ishara hizi hufanyika kwa sababu ovari zako zinaacha kutengeneza mayai, na mwili wako unatengeneza viwango vya chini vya homoni aina 'oestrogen' na 'progesterone'. Ishara hizi zitatokomea mwili wako unapoendelea kuzoea viwango vidogo vya 'oestrogen'.

Hisia za mwanamke kuhusu kuisha kwa siku za hedhi hutegemea sana athari za mabadiliko haya mwilini mwake. Pia hutegemea maoni ya jamii yake kuhusu akina mama wazee. Atafurahia kutokuwa tena na siku za hedhi, lakini atahisi huzuni kwani hawezi tena kupata watoto.

Sources
  • Burns, A. A., Niemann, S., Lovich, R., Maxwell, J., & Shapiro, K. (2014). Where women have no doctor: A health guide for women. Hesperian Foundation.
  • Audiopedia ID: sw010902