Je ni vipi ambavyo usafi pale nyumbani huzuia magonjwa

From Audiopedia - Accessible Learning for All
Jump to: navigation, search
QR for this page

https://www.audiopedia.org/Je_ni_vipi_ambavyo_usafi_pale_nyumbani_huzuia_magonjwa

Kwa vile watu wa familia moja hushirikiana kwa karibu, ni rahisi sana kusambaza viini na magonjwa kwa familia nzima.

Familia haitakuwa na maambukizi ikiwa:

  • wataosha vyombo wanavyotumia kwa kula kwa sabuni (au kwa kutumia jivu) na maji masafi baada ya kuvitumia. Ikiwezekana, waviache vyombo hivi vikauke kwenye jua (jua huua viini vinavyosababisha magonjwa).
  • wasafishe nyumba kila mara. Wafagie na kuosha sakafu zote, kuta na chini ya viti. Wazibe nyufa na mashimo kwenye sakafu au kuta, ambapo mende, kunguni na nge hujificha.
  • anika malazi kwenye jua ili kuua vijidudu na kunguni.
  • usiteme mate sakafuni. Funika mdomo kwa kutumia mkono wako au kitambaa cha mkononi unapokohoa au kupiga chafya. Ikiwezekana, osha mikono yako.


Sources
  • Burns, A. A., Niemann, S., Lovich, R., Maxwell, J., & Shapiro, K. (2014). Where women have no doctor: A health guide for women. Hesperian Foundation.
  • Audiopedia ID: sw010112