Nifanye nini nikipata uvimbe kwenye matiti yangu
From Audiopedia - Accessible Learning for All
QR for this page
Ikiwa uvimbe wenyewe ni laini na unasonga kwa urahisi kama mpira unapousukuma kwa vidole vyako, usiwe na wasiwasi. Ikiwa uvimbe huo ni mgumu, na hauna muundo kamili, hauna uchungu, endelea kuchunguza - hasa ikiwa uvimbe huo uko kwenye titi moja peke yake na hausongi unapousogeza. Muone daktari ikiwe uvimbe huo bado utakuwepo baada ya hedhi. Huenda hii ni dalili ya saratani. Unatakiwa utafute ushauri wa kimatibabu ikiwa titi linavuja damu au usaha.